Shirika la habari la Ufaransa limeripoti kuwa barua hiyo ambayo imetumwa kwa msikiti wa Ayyub Sultan inakipengee kinachowaambia Waislamu 'ondokeni katika nchi yetu la sivyo tutakufukuzeni sisi wenyewe'.
Msemaji wa Waislamu wa Strasbourg Yahya Nalband amesema kuhusu hatua hiyo ya kibaguzi kwamba kandokando ya barua hiyo kulikuwa na ukurasa uliochomwa moto nusu wa kitabu kitukufu cha Qur'ani. Watumaji wa barua hiyo pia wametishia kuwaua Waislamu.
Yahya Nalband amesema kuwa polisi ya Ufaransa inafanya uchunguzi wa kuwatia nguvuni watu waliohusika na kitendo hicho cha kibaguzi.
Katika sehemu nyingine ya matamshi yake, msemaji wa msikiti wa Strasbourg amesema Waislamu wa Ufaransa wanalaani vikali kitendo hicho na wanaelewa kwamba kinafanyika kwa lengo la kutia tashwishi katika fikra zao. Amesisitiza juu ya kuchukuliwa hatua za kupambana na watu wanaofanya vitendo kama hivyo. 695340