IQNA

Mara hii Kasisi Terry Jones ataka maandamano yafanyike siku ya Idul Haji

11:50 - November 16, 2010
Habari ID: 2033010
Terry Jones kasisi wa Kimarekani aliyechochea hivi karibuni harakati ya dharau dhidi ya Qur'ani Tukufu kwa kutaka kitabu hicho kitakatifu kichomwe moto mara hii ametaka Wakristo wafanye maandamano ya malalamiko katika siku ya Idul Adh'ha ikiwa ni katika juhudi zake za kujipatia umashuhuri duniani.
Kasisi huyo mchochezi na anayekosea heshima mara kwa mara matukufu ya Kiislamu na Waislamu, mara hii amechukua hatua ya kuchekesha ya kuwataka Wakristo wakusanyike katika eneo yalipokuwa majengo pacha mjini New York katika siku ya Idul Adh'ha ili kudhihirisha malalamiko yao dhidi ya Waislamu wanaodaiwa kuwa ndio waliohusika na milipuko ya Septemba 11, 2001 katika eneo hilo. Katika matamshi mengine ya kijahili, kasisi huyo amedai kwamba Misri ni nchi ya Wakristo wa Kikopti ambayo ilitekwa nyara na kukaliwa kwa mabavu na Waislamu. Ametaka Mayahudi wawafukuze Waislamu katika mji wa Beitul Muuqaddas huko Palestina inayokaliwa kwa mabavu na Wazayuni na kuuteka tena kikamilifu mji huo.
Kasisi huyo mchochezi pia amewataka wakazi wa kusini mwa Sudan wafanye juhudi za kujitenga na serikali ya kaskazini na kuanzisha nchi na serikali mpya ya Kikristo katika eneo hilo. 696213
captcha