IQNA

Mashindano ya Kimataifa ya Qurani ya Wanachuo Waislamu huleta Umoja wa Kiislamu

12:35 - November 26, 2010
Habari ID: 2037312
Ubunifu wa Iran wa kuwakusanya pamoja wanafunzi wa vyuo vikuu vya Kiislamu duaniani kwa ajili ya mashindano ya Qurani imetajwa kuwa hatua muhimu katika kuleta umoja wa Kiislamu duniani.
Hayo yamesemwa na Mkuu wa Taasisi ya Jihad ya Vyuo Vikuu nchini Iran Bw. Mohammad Yadegari. Akizungmza na IQNA, amesema kuwa, ‘kwa maoni yangu mashindano kama haya yanaweza kuwa na nafasi muhimu ya kustawisha mabadilishano ya mawazo baina ya wanachuo kutoka nchi mbali mbali jambo ambalo bila shaka litakuwa na matunda mema’.
Yadegar amesema kuwa maadui wanatumia kila mbinu kutoa taswira potofu kuhusu Jamhuri ya Kiislamu duniani na kwa kuzingatia hilo, ‘mashindano ya Kimataifa ya Qurani Tukufu nchini Iran yanaweza kuwa na nafasi muhimu kuvunja njama hizo za maadui’.
Mashindano ya Tatu wa Kimataifa ya Qurani Tukufu ya Wanachuo Waislamu yatafanyika Januari 19-22 mwaka 2011 katika mji mtakatifu wa Mashhad.
699670
captcha