Hujjatul Islam Hamid Mohammadi Naibu Waziri wa Utamaduni na Miongozo ya Kiislamu anayehusika na masuala ya Qur'ani amesema kuzingatiwa zaidi tafsiri ya Qur'ani kutainua kiwango cha mashindano hayo.
Amesisitiza kuwa vyanzo vya tafsiri vinapaswa kuchaguliwa miongoni mwa tafsiri zinazokubaliwa kwa pamoja na madhehebu ya Shia na Suni.
Amesema kuwa mashindano hayo ni fursa nzuri ya kuarifisha utambulisho wa Qur'ani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
Mashindano ya Tatu ya Kimataifa ya Qurani ya Wanachuo Waislamu yatafanyika katika mji wa Mash'had kaskazini mashariki mwa Iran mwezi ujao wa Januari 9-11.
706686