IQNA

Warsha ya masomo ya kutadabari Qur'ani Tukufu kufanyika Saudia

16:37 - December 13, 2010
Habari ID: 2047496
Warsha ya masomo ya kutadabari Qur'ani Tukufu imepangwa kufanyika huko Riyadh mji mkuu wa Saudi Arabia mwezi Januari mwakani.
Kwa mujibu wa gazeti la al-Bilaad, warsha hiyo inadhaminiwa na Wizara ya Wakfu na Masuala ya Kiislamu na Uhubiri ya Saudi Arabia kwa ushirikiano wa Idara Kuu ya Jumuiya za Masuala ya Kheri na Hifdhi ya Qur'ani ya nchi hiyo.
Mkuu wa Idara hiyo Uthman bin Muhammad as-Swidiqi amesema kuhusiana na suala hilo kwamba warsha hiyo itafanyika kwa lengo la kuwasilisha maana halisi ya Qur'ani, kuimarisha uhusiano kati ya wanachuo wanaosoma masomo ya Qur'ani, kutekeleza mafundisho ya Qur'ani kupitia masomo katika ngazi mbalimbali na kujipamba kwa maadili ya Qur'ani. 711738
captcha