Taasisi ya Qur'ani ya Afrika Kusini imeripoti kuwa masomo hayo yatakuwa yakitolewa kuanzia Jumatatu hadi Ijumaa kwa wanafunzi wa kike na kiume. Ripoti hiyo imesema kuwa watoto hao watapewa mafunzo ya Qur'ani na maarifa ya kitabu hicho.
Ripoti hiyo imesema kuwa watoto hao kwanza watafundishwa sheria za tajwidi, kiraa na mbinu za kuhifadhi Qur'ani Tukufu.
Vilevile watapewa mafunzo ya lugha ya Kiarabu kwa ajili ya kuelewa vyema Qur'ani Tukufu na elimu mbalimbali za Kiislamu.
Watoto wenye juu ya umri wa miaka mitatu watakaoshiriki katika masomo hayo wataweza kusoma Qur'ani Tukufu na kuhifadhi aya zake baada ya kukamilisha masomo hayo.
Masomo hayo ambayo yanafanyika kwa lengo la kuwafundisha watoto utambulisho wa Kiislamu yataendelea kwa kipindi cha mwaka mzima. 720036