Kongamano hilo ambalo litawajumuisha wanafikra na wasomi wa Kiislamu katika uwanja wa vyombo vya habari kutoka kote ulimwenguni limepangwa kufanyika katika Chuo Kikuu cha Kadir Has na Taasisi ya Kimataifa ya Utafiti wa Vyombo vya Habari na Mawasiliano IAMCR.
Kongamano hilo la siku tano litajadili masuala mbalimbali yakiwemo ya Uislamu; mawasiliano na mazungumzo ya tamaduni, Uislamu; zama za dijitali na uvumbuzi, Uislamu; uhai mpya na uraia, sura ya Uislamu na Waislamu katika vyombo vya habari vya kimataifa, sura ya wasio Waislamu katika vyombo vya habari vya Kiislamu, vyombo vya habari vya kijamii na uvumbuzi wa vijana wa Kiislamu, usanii na utamaduni wa ulimwengu wa Kiislamu na Ulaya na Uislamu; nafasi ya vyombo vya habari. 722869