IQNA

Ensaiklopidia ya waandishi wa Kiislamu kuchapishwa

10:50 - January 16, 2011
Habari ID: 2065071
Ensaiklopidia ya kwanza ya waandishi wa Kiislamu itachapishwa na Kituo cha Utafiti, Utamaduni na Sayansi za Kiislamu cha Iran.
Kituo hicho kimetangaza kuwa watafiti wake watakusanya biografia na bibiliografia ya wasomi wa karne tatu za kwanza hijria katika juzuu ya kwanza ya ensaiklopidia hiyo.
Orodha ya majina ya waandishi itawekwa kwa mpangilio wa alfabeti. Maelezo kuhusu kila mwandishi yatajumuisha siku na mahala pa kuzaliwa, elimu, safari za kielimu, waalimu na wanafunzi wake pamoja na harakati zake za kijamii na kisiasa.
730693

captcha