IQNA

Mashindano ya Kimataifa ya Qur'ani kufanyika Qatar

16:04 - January 17, 2011
Habari ID: 2066263
Mashindano ya Kimataifa ya Kiraa ya Qur'ani Tukufu maalumu kwa vijana wenye umri wa miaka 9-12 yatafanyika Qatar kwa himaya ya Kanala ya Televisheni ya Watoto ya Al Jazeera ikishirikiana na Wizara ya Waqfu na Masuala ya Kiislamu ya Qatar.
Kwa mujibu wa gazeti la Al Sharq linalochapishwa Qatar, mashindano hayo yatawashirikisha vijana wa kike na kiume kutoka nchi mbalimbali za Kiislamu.
Kamati ya kuandaa mashindano hayo imesema nukta zitakazozingatiwa ni pamoja na sheria za tajwid na umaridadi wa sauti na lahni na kila mshiriki atapewa dakika tatu kuonyesha ustadi wake katika kiraa.
Wanaotaka kushiriki katika mashindano hayo wanapaswa kujiandikisha kabla ya tarehe tano Februari katika tovuti ya Islamweb.
Jopo la majaji katika mashindano hayo linajumuisha maulamaa na wataalamu wa Qur'ani Tukufu.
732068
captcha