Tovuti ya "map.ma" imeripoti kuwa mkutano huo ambao utamalizika kesho unahudhuriwa na wanaharakati wa haki za binadamu, wanadiplomasia wa nchi za kigeni, wanasiasa na wasanii.
Miongoni mwa masuala yanayojadiliwa katika mkutano huo ni pamoja na suala la kuundwa muungano wa kimataifa wa haki za binadamu kwa ajili ya kuwatetea mateka wa Kipalesina katika jela za utawala ghasibu wa Israel.
Mkutano huo unafanyika chini ya anwani ya "Kukomboa Mateka wa Kipalestina, Wajibu wa Kimataifa. 734529