IQNA

Kikao cha 'Uislamu na upotofu wa Magharibi' kufanyika Brussels

14:14 - February 08, 2011
Habari ID: 2077587
Kikao cha 'Uslamu na Upotofu wa Magharibi' kimepangwa kufanyika mjini Brussels Ubelgiji Jumamosi tarehe 12 Februari.
Kwa mujibu wa tovuti ya Islamic-events.be, kikao hicho kitafanyika katika Kituo cha Utamaduni, Uislamu na Masomo cha al-Hikma kuanzia saa nane alasiri. Mkuu wa Kituo cha Kiislamu cha Geneva pia atashiriki katika kikao hicho.
Kikao cha Utamaduni na Kiislamu cha al-Hikma ni kituo kisicho cha kiserikali ambacho kinajishughulisha na masuala mbalimbali ya kidini, kiutamaduni, kijamii, kifamilia na kimasomo. Uandaaji wa mikutano, huduma za masomo ya kidini na kifamilia, intaneti, vipindi tofauti vya masomo, michezo na huduma za maktaba ni shughuli nyingine zonazofanywa na kituo hicho. 743792
captcha