IQNA

Mashindano ya Qur'ani na Hadithi ya wanachuo wa kigeni Iran

16:23 - February 15, 2011
Habari ID: 2081023
Washiriki kutoka nchi 21 watashiriki katika duru ya pili ya "Mashindano ya Qur'ani na Hadithi maalumu kwa wanachuo wa kidini wasiokuwa Wairani" yatakayofanyika katika Chuo Kikuu cha Imam Khomeini kuanzia Februari 19-20.
Mashindano hayo yatakayoendelea kwa muda wa siku mbili yana jumuisha makundi 30 ya washiriki kutoka nchi 21.
Chuo Kikuu cha Imam Khomeini kinafungamana na Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Al Mustafa.
Abdul Reza Sharifi Mkurugenzi wa Idara ya Qur'ani na Hadithi katika Chuo Kikuu cha Imam Khomeini amesema awamu hii ya mashindano imeshuhudia ongezeko kubwa la washiriki ikilinganishwa na mwaka jana.
Ameongeza kuwa mashindano hayo yatajumuisha qiraa, hifdhi, adhana na dua.
746704

captcha