IQNA

Mashindano ya Qur'ani katika jimbo la British Columbia, Canada

17:21 - February 16, 2011
Habari ID: 2082212
Muungano wa Waislamu wa Canada na Kituo cha Habari cha Kiislamu vitafanya mashindano ya 10 ya Qur'ani katika jimbo la British Columbia nchini Canada.
Kituo cha habari cha bcmuslims kimeripoti kuwa mashindano hayo yatafanyika Aprili 16 na 17 katika awamu mbili za utangulizi na awamu ya mwisho.
Mashindano hayo yatajumuisha hifdhi ya Qur'ani na watu wa umri tofauti wanaruhusiwa kushiriki.
Muhula wa mwisho wa kujiandikisha ni tarehe 3 Aprili.
Zawadi nono zitatolewa kwa washindi wa mashindano hayo. 749021

captcha