Kwa mujibu wa gazeti la Qatar la as-Sharq, mashindano hayo yatakayofanyika katika Klabu ya Michezo ya al-Arabi ya mjini Doha, kati ya tarehe 27 Februari hadi 8 Machi yatawashirikisha washindani 65 kutoka taasisi na vituo 16 vya vijana wa Qatar.
Akizungumzia suala hilo Jamal Faizi mkuu wa kitengo kilichotajwa amesema kuwa mashindano hayo yatafanyika katika fremu ya shughuli za kuchaguliwa Doha kuwa mji mkuu wa kiutamaduni wa ulimwengu wa Kiislamu katika mwaka uliopita wa 2010. 751686