Kwa mujibu wa mwandishi wa IQNA, tarjumi hiyo itazinduliwa na Bw. Mohammad Baqer Khorramshad Mkuu wa ICRO na Hujjatul Islam Rabbani Mkurugenzi wa Taasisi ya Andishe-ye-Sharq, mtarjumi, wataalamu wa utamaduni na wataalamu na wanafunzi wa lugha ya Kihispania.
Tarjumi hiyo imechapishwa na Kituo cha Tartjumi na Uenezi wa Mafundisho ya Kiislamu kwa ushirikiano na Taasisi ya Andishe-ye-Sharq.
Baada ya kuzinduliwa tarjumi hiyo kutakuwa na kikao cha kutathmini tarjumi ya "Kitabu cha Nne cha Mathnawi" na “Bar Karane-ye Chehel Hadith” kilichoandikwa na Imam Khomeini MA. Kikao hicho pia kitachunguza Tarjumi ya Kiingereza ya "Dastan-e-Rastan" na "Imam Ali AS na Amani ya Dunia" .
759448