IQNA

Mfumo wa kifedha wa Kiislamu wajadiliwa Russia

13:50 - March 08, 2011
Habari ID: 2092111
Baada ya wasomi nchini Russia kukubali mfumo wa kifedha wa Kiislamu sasa imebakia wanasiasa na maafisa wa serikali kutambua umuhimu wa mfumo wa kifedha wa Kiislamu na nafasi yake muhimu hasa baada ya mgogoro wa kifedha duniani
Imetambulika kuwa mfumo wa kifedha wa Kiislamu ndio njia bora zaidi kwa Russia na Nchi za Jumuiya ya Madola Huru CIS (Nchi zilizokuwa Shirikisho la Sovieti kabla ya kupata uhuru).
Katika mkutano kuhusu 'Mfumo wa Kifedha wa Kiislamu Russia na CIS' uliofanyika wiki iliyopita mjini Istanbul, masuala kuhusu mfumo wa kifedha wa Kiislamu yalijadiliwa.
Kati ya nchi za CIS ni Tajikistan na Kazakhstan zilizotangaza kuwa tayari kuanzisha mfumo wa kifedha wa Kiislamu.
Kikao hicho kimeonelea kuwa kuna haja ya kuwaelimisha maafisa wa kifedha wa Russia na CIS kuhusu mfumo wa kifedha wa Kiislamu.
759401

captcha