IQNA

Kikao cha Seerah ya Mtume chafanyika Jordan

0:34 - April 04, 2011
Habari ID: 2099990
Kikao cha ‘Seerah ya Mtume na Tabia za Muislamu’ kimefanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Fikra za Kiislamu huko Jabal al Weibdeh nchini Jordan.
Kwa mujibu wa gazeti la Jordan Post, kikao hicho kilianza Aprili Pili kwa ushirikiano wa Jumuiya ya Kuhuisha Hadithi na Turathi Jordan.
Wasomi 22 kutoka Jordan, Saudi Arabia, Sudan, Iraq na Kuwait wanashiriki katika kikao hicho ambacho kinajadili umuhimu wa Seerah ya Mtume SAW katika kukuza shakhsia ya Muislamu.
Fathi Malkawi, mmoja wa waandalizi amesema washiriki watajadili pia namna marejeo ya Seerah yanaweza kutumiwa katika malezi ya Muislamu.
Kikao hicho kimemaliza kazi zake Aprili tatu.
767960

captcha