Katika taarifa yao Wabunge zaidi ya 200 wamesema leo ulimwengu wa Kiislamu unaomboleza mauaji ya kinyama dhidi ya raia huko Libya, Yemen na Bahrain.
Wamesema kuwa nchi za Magharibi zinazodai kutetea haki za binaadamu zimepuuca na kunyamazia kimya mauaji ya kinyama katika eneo na kuongeza kuwa jinai hizo zinafanyika kwa uungaji mkono wa moja kwa moja wa Marekani na Uingereza.
Wabunge wa Iran wameitaka Saudi Arabia kuondoa vikosi vyake vamizi nchini Bahrain.
769984