Hatua ya mwisho ya duru ya tano ya mashindano ya hifdhi ya Qur'ani Tukufu yaliyopewa jina la Rashid al-Mualla, ambayo ni maalumu kwa wanafunzi wa shule za serikali na binafsi yamepangwa kufanyika tarehe Mosi Mei huko katika mji wa Umm al-Qiwein katika Umoja wa Falme za Kiarabu.
Mashindano hayo yatafanyika katika hatua tano ambapo hatua ya kwanza itawahusu watoto wadogo wa shule za chekechea. Hatua ya pili itawahusisha wanafunzi wa madarasa ya chini ya shule za msingi ambao watatakiwa kuhifadhi juzuu moja ya Qur'ani kisha hatua ya tatu itakuwa ni ya wanafunzi wa madarasa ya juu ambao watatakiwa kuhifadhi juzuu mbili. Wanafunzi wa shule za sekondari watashindana katika kuhifadhi juzuu tatu ilihali hatua ya mwisho itawahusisha wanafunzi wote waliohitimisha hifdhi ya juzuu tano za Qur'ani Tukufu. 771144