IQNA

Mwanasiasa wa Uingereza aivunjia heshima Qurani

14:46 - April 11, 2011
Habari ID: 2104132
Mwanasiasa mwingine mwandamizi wa Uingereza mwenye misimamo mikali ameivunjia heshima Qurani Tukufu kama njia ya kupata uungaji mkono wa wafuasi wa chama chake.
Sion Owens mwanachama mwandamizi wa chama cha BNP na mgombea kiti katika uchaguzi wa bunge la eneo la Welsh ametiwa nguvuni akichoma moto Qurani Tukufu katika bustani lake.
Hivi sasa wanasiasa wenye misimamo mikali Ulaya na Marekani wanachezea hisia za wafuasi wao kwa kueneza chuku dhidi ya Waislamu na Uislamu katika jamii ambazo zinawachukia wageni.
Mwanasiasa huyo wa mrengo wa kulia nchini Uingereza anapanda wimbi la chuki dhidi ya Uislamu miongoni mwa watu wasio na elumu nchini Uingereza wasio fahamu mafundisho ya Kiislamu.
Kumekuwepo na ongezeko la chuki dhidi ya Uislamu katika nchi za Maghairbi ambazo zimechochewa na wanasiasa wanaotafuta kisingizio cha kufeli sera zao za kiuchimi na kijamii.
772419
captcha