IQNA

Mashindano ya Qurani ya familia za Mashahidi kufanyika Tehran

14:53 - April 11, 2011
Habari ID: 2104137
Mashindano ya 23 ya mikoani ya Qurani Tukufu maalumu kwa familia za mashahidi na wanaojitolea yatafanyika Aprili 15 mjini Tehran.
Kwa mujibu wa Idara ya Habari ya Shirika la Mashahidi na Wanaojitolea, watu 150 waliofanikiwa wilayani watashiriki katika mashindano ya mikoa.
Mashindano hayo yanajumuisha Tarteel, Qiraa, utafiti na tafsiri ya Qurani Tukufu.
Jopo la majaji katika maonyesho hayo litajumuisha wataalamu wa kimataifa wa Qurani Tukufu.
Washindi watashiriki katika kozi ya miezi miwili itakayowatayarisha kushiriki kikamilifu katika mashindano ya kitaifa.
772155
captcha