Kwa mujibu wa mwandishi wa IQNA nchini Zambia, kozi hizo zitafanyika kwa ajili ya watoto na vile vile watu wazima wenye uwezo duni wa kifedha katika miji mbali mbali nchini humo ikiwemo Katuba.
Shirika la Utamaduni na Mahusiano ya Kiislamu la Iran litatoa suhula zinazohitajika katika kozi hizo ikiwa ni pamoja na waalimu.
Washiriki watafundishwa hifdhi na qiraa ya Qurani Tukufu. Mafundisho hayo yanafanyika kwa lengo la kueneza utamaduni wa Qurani Tukufu katika maeneo husika.
771694