IQNA

Hatua ya mwisho ya mashindano ya kimataifa ya hifdhi ya Qur'ani yaanza Senegal

16:35 - April 11, 2011
Habari ID: 2104202
Hatua ya mwisho ya mashindano ya kimataifa ya hifdhi na tajwidi ya Qur'ani Tukufu mahsusi kwa wasomaji na mahafidh wa Qur'ani kutoka bara la Afrika ilianza jana tarehe 10 Aprili huko Dakar mji mkuu wa Senegal.
Mashindano hayo yaliyopangwa kuendelea kwa siku nne yameandaliwa na Jumuiya ya Kimataifa ya Hifdhi ya Qur'ani kwa ushirikiano wa Jumuiya ya Kiislamu ya Senegal. Akibainisha malengo ya mashindano hayo, Abdallah Basifr, Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Hifdhi ya Qur'ani amesema kwamba malengo hayo ni pamoja na kuvutia uzingatiaji wa Qur'ani na kuwashawishi vijana wa Kiafrika wahifadhi, kusoma na kutadabari kitabu hicho kitakatifu. 771537
captcha