Tamasha hilo lililoandaliwa na Ofisi ya Shahid Sadr kwa ushirikiano wa Kamati ya Uungaji Mkono kwa Qur'ani Tukufu ya Iraq, lilifanyika katika mtaa wa Sadr mjini humo. Tamasha hilo lililoandaliwa hapo siku ya Ijumaa lilihudhuriwa na wanazuoni, wanafikra wa Kislamu, wasomaji Qur'ani na wanasiasa wa nchi hiyo. Wabunge waliohudhuria tamasha hilo wamesema kuwa bunge la Iraq limeutaja mwaka huu kuwa mwaka wa Qur'ani Tukufu ikiwa ni katika kutetea kitabu hicho kitakatifu na kulaani kitendo cha kasisis Terry Jones cha kukosea heshima kitabu hicho. 775164