Ayatullahil Udhma Syyid Ali Sistan, mar'ja taqlidi wa Mashia amekataa ombi la mfalme wa Saudi Arabia la kufanya naye mazungumzo ya simu baada ya askari wa nchi hiyo kushirikiana na askari wa ufalme wa Aal Khalifa wa nchini Bahrain kukandamiza na kuwaua ovyo wananchi wa nchi hiyo wanaofanya maandamano ya amani ya kupigania haki zao.
Ayatullah Sistani amelaani vikali jinai zinazofanywa na askari wa Saudia dhidi ya taifa la Bahrain na kusema kuwa jambo hilo linakwenda kinyume na maslahi ya watu wa nchi hiyo. Akizungumzia jambo hilo hivi karibuni, Sayyid Jawad Shahrestani, mwakailishi wa marja huyo katika Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa kiongozi huyo wa kidini amehuzunishwa sana na matukio ya Bahrain na kwamba anafanya juhudi kubwa za kupunguza machungu ya wananchi wa nchi hiyo wanaoendelea kukandamizwa na kuuawa ovyo na askari wa Saudi Arabia wakishirikiana na wa utawala wa Manama. Amesema Ayatullah Sistani anatambua vyema ushirikiano na uhusiano mkubwa uliopo baina ya koo mbili dhalimu za Saudi na Aal Khali. 775156