Pembizoni mwa duru ya tatu ya safari za Rais Mahmoud Ahmadinejad wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika mkoa wa Kurdistan magharibi mwa Iran, tawi la Chuo Kikuu cha Madhehebu ya Kiislamu kimefunguliwa Aprili 20.
Sherehe za ufunguzi zimehudhuriwa na Waziri wa Utamaduni na Muongozo wa Kiislamu Dr. Sayyed Mohammad Husseini ambaye ametoa hotuba iliyodhudhuriwa na wasomi, wanazuoni wa Kiislamu na wanaharakati wa Qurani.
Kuanzishwa chuo hicho ni katika sera za Jamhuri ya Kiislamu ya Iran za kustawisha umoja wa Kiislamu kupitia utafiti na masomo yanayolenga kuleta maelewano baina ya madhehebu ya Kiislamu.
Aidha katika safari ya rais Ahmadinejad mkoani Kurdishatan taasisi 30 za kiutamaduni zinazofungamana na misiki zimefunguliwa.
777738