Mwenyekiti wa Kamati ya Tuzo ya Kimataifa ya Qur'ani ya Dubai Ibrahim Muhammad Bumalha amesema kuwa mashindano hayo yanaanza leo alasiri mjini Dubai na kwamba zawadi nono zitatolewa kwa washindi.
Amesema kuwa washindan 493 wa rika zote wanashiriki katika mashindano hayo.
Ahmad Saqar al Suwaidy ambaye ni miongoni mwa wanachama wa kamati hiyo amesema mashindano hayo yanawashirikisha watoto wadogo, vijana na maimamu wa misikiti.
Awamu ya mwisho ya mashindano ya kiraa bora zaidi ya tartili itafanyika tarehe 15 Mei katika msikiti wa Hassan Sheikh mjini Dubai. 779694