IQNA

Sisitizo la kubuniwa Baraza Kuu la Mashia Saudi Arabia

14:03 - April 25, 2011
Habari ID: 2111607
Wanafikra wa Kiiskamu waliohudhuria mkutano wa wanaharakati wa Kishia katika mji wa Qatif nchini Saudi Arabia wamesisitiza juu ya udharura wa kubuniwa Baraza Kuu la Waislamu wa madhehebu ya Shia wa nchi hiyo.
Wanazuoni na maulama waliohudhuria kikao hicho wamesema kuwa kutokuwepo kwa baraza kama hilo ndilo tatizo na changamoto kuu inayoikabili jamii ya Mashia wa Saudi Arabia na kutaka hati madhubuti ibuniwe kwa lengo la kueneza uhuru wa kifikra, haki za binadamu na uhuru kati ya raia na Waislamu wote wa nchi hiyo.
Juhudi za kulea kizazi bora kinachofahamu vyema utamaduni wa Kiislamu, kuondoa hitilafu miongoni mwa wanazuoni na kuzingatia mielekeo ya kuvumiliana kwenye jamii ni masuala mengine yaliyojadiliwa katika kikao hicho. 779704
captcha