IQNA

Mkutano wa Kimataifa wa ‘Dini, Haki za Binadamu na Wanawake’ kufanyika Tehran

13:38 - April 28, 2011
Habari ID: 2113429
Shirika la Iran la Utamaduni na Mahusiano ya Kiislamu ICRO limepanga kongamano la kimataifa kuhusu ‘Dini, Haki za Binadamu na Wanawake’ litakalofanyika Aprili 30 mjini Tehran.
Kwa mujibu wa Idara ya Wanawake na Masuala ya Familia ya ICRO, kongamano hilo litahudhuriwa na taasisi zisizo za kiserikali kutoka nchi kadhaa. Washiriki wanatazamiwa kutangaza mshikamano wao na harakati ya mwamko wa Kiislamu.
Kati ya nchi zitakazoshiriki ni pamoja na Algeria, Tunisia, Lebanon, Sudan, Iraq, Syria, Marekani, Japan, Bahrain na Argentina pamoja na mashirika 50 yasiyo ya kiserikali ya wanawake wa Iran na wale kutoka jamii za waliowachache.
Kikao hicho kitamalizika kwa taarifa ya kuunga mkono harakati ya mwamko wa Kiislamu.
782140
captcha