IQNA

Waislamu Afrika Kusini wajadili Sheria ya Ndoa za Kiislamu

11:41 - May 01, 2011
Habari ID: 2114820
Waislamu nchini Afrika Kusini wanaendelea kujadili rasimu ya sheria ya ndoa za Kiislamu. Inatazamiwa kuwa sheria hiyo ikipitishwa ndoa za Waislamu zitatambuliwa rasmi nchini Afrika Kusini.
Waziri wa Sheria wa Afrika Kusini Jeff Radebe amesema maoni na mapendekezo kuhusu rasimu ya muswada wa sheria hiyo yatapokelewa hadi Mei 31.

Jumuiya ya Mawakili Waislamu ya Afrika Kusini imepinga sheria hiyo na kuitaja kuwa inayokiuka sheria za Kiislamu kwa sababu inaruhusu mahakama zisizo za Kiislamu kutatua migogoro ya ndoa za Waislamu. Jumuiya ya Wanawake Waislamu ya Afrika Kusini pia imepinga sheria hiyo.

Taasisi kadhaa za Kiislamu nchini Afrika Kusini zimetaka serikali ianzishe mahakama maalumu za Kiislamu ambazo zitashughulikia masuala ya ndoa za Waislamu.
783766
captcha