IQNA

Kikao cha kujadili 'Tarjumi za Kiingereza za Qur'ani' Tehran

15:27 - May 02, 2011
Habari ID: 2116015
Kikao maalumu cha kujadili 'Tarjumi za Kiingereza za Qur'ani' kitafanyika Mei Tatu katika Shirika la Habari za Qur'ani la Kimataifa IQNA lenye makao yake mjini Tehran.
Hiki ni kikao cha kwanza katika mfululizo wa vikao kuhusu mada hii.
Dkt. Salar Manafi na Dr. Hussein Mollanazar ni kati ya watakaohudhuria kikao hicho ambacho kimeandaliwa kwa ushirikiano na Chuo Kikuu cha Mafunzo na Sayansi za Qur'ani.
Kikao hicho kitakuwa huru kwa wale wote wanaohusika na masuala ya Qur'ani au wasomaji wa kawaida.
784875
captcha