IQNA

Darsa 7000 za tafsiri ya Qur'ani katika misikiti ya Iran kila siku

17:40 - May 02, 2011
Habari ID: 2116038
Katibu wa Taasisi ya Misikiti Iran amesema kuna darsa 7000 za tafsiri ya Qur'ani ambazo hufanyika kila siku katika misikiti nchini Iran.
Akizungumza katika kikao cha Mpango wa Tilawat Noor, Hujjatul Islam Hamid Reza Arbab Suleimani ameongeza kuwa kusoma Qur'ani tu hakutoshi. Amongeza kuwa, 'ni kweli kuwa hata kuangalia aya za Qur'ani kuna thawabu lakini ukweli ni kuwa Qur'ani iliteremshwa kumuongoza mwanadamu kutoka gizani kuelekea katika nuru. Moja ya njia za kuhakikisha mwanadamu anapata muongozo ni kustawisha utamaduni wa kufasiri Qur'ani'.
Ameongeza kuwa hii leo kuna tafsiri kadhaa za Qur'ani ambazo zinaweza kuwaongoza wale wanaotaka kupata mafunzo ya Qur'ani.
784052
captcha