Mohammad Bonyadi ambaye ni mkurugenzi mkuu wa Idara ya Qur'ani na Sala katika Wizara ya Elimu amemuambia mwandishi wa IQNA kuwa warsha hizo zitaanza mwaka mpya wa kiakademia ambao kwa kawaida huanza mwezi Septemba nchini Iran.
Amesema shule zote za msingi na sekondari zimeshurutishwa kuandaa warsha hizo pamoja na mashindano wa Qur’ani na Sala katika mwaka mpya wa kiakademia.
Kwa mujibu wa Wizara ya Elimu, warsha hizo zitajumuisha mada kama vile hotuba za Qur’ani, hadithi za Qur’ani, tafsiri na tarjumi ya Qur’ani, mashairi ya Qur’ani n.k.
789824