Kituo hicho kimefunguliwa katika sherehe iliyohudhuriwa na Nidhal al Ibadi ambaye ni mjumbe wa Baraza la Idara ya Jumuiya ya Kulinda Qur'ani Tukufu.
Mkuu wa jumuiya hiyo katika eneo la al Aqaba Umar Said amewashukuru watu waliojitolea kujenga kituo hicho cha Qur'ani na kupongeza jumuiya yake kwa kutoa huduma nzuri za Qur'ani.
Amesema Jumuiya ya Kulinda Qur'ani ya Jordan imetoa huduma kubwa katika masuala ya Qur'ani ikiwa ni pamoja na kuanzisha vituo 800 vya Qur'ani nchini Jordan, kutoa elimu na mafunzo ya Qur'ani kwa wanafunzi 8 waliohitimu masomo na makarii 100, kuwa na wanachama 25 elfu ambao ni wanafunzi, kuchapisha nakala elfu 7 za jarida la al Furqan na tasiri ya Qur'ani kwa lugha ya ishara. 792467