Kongamano hilo limeandaliwa na Kitengo cha Mafunzo ya Kiislamu na litajadili mbinu za utafiti wa Qur'ani na masuala ya afya na vilevile mtazamo wa Qur'ani kuhusu mwanadamu.
Ali Gholami Dehaghi katibu wa kongamano hilo amesema utafiti wa Qur'ani unalenga kufahamu zaidi hekima ya Qur'ani.
Amesema kuwa mtazamo wa Qur'ani kuhusu maadili ya kikazi kwa wanaofanya kazi katika sekta ya afya, mafundisho ya Qur'ani na afya ya kisaikolojia, uhusiano baina ya sayansi na dini kwa kuzingatia Qur'ani na afya, mfumo wa afya kwa mtazamo wa Qur'ani na mtazamo wa Qur'ani kuhusu uadilifu katika afya ni kati ya mambo yatakayojadiliwa katika kongamano hilo la siku mbili.
793224