IQNA

Vikao vya Qur'ani kufanyika katika makanisa ya Marekani

19:03 - May 18, 2011
Habari ID: 2124716
Viongozi wa makanisa ya Marekani wametangaza kuwa wataandaa vikao vya Qur'ani na vitabu vingine vya mbinguni katika makanisa ya nchi hiyo mwezi Juni kwa madhumuni ya kupambana na ubaguzi na chuki dhidi ya Uislamu na vilevile kuimarisha ushirikiano kati ya wafuasi wa dini tofauti.
Vikao hivyo ambavyo vitafanyika chini ya anwani ya 'Itikadi za Pamoja; Umoja katika Maombi na Maelewano' vitaandaliwa na Taasisi ya Dini na Haki za Binadamu ya mjini Washington DC.
Vikao hivyo vinaandaliwa kwa shabaha ya kuimarisha urafiki na ushirikiano kati ya wafuasi wa dini za Kiislamu, Kikristo, Kiyahudi na dini nyinginezo za mbinguni.
Waandaaji wa vikao hivyo wanasema kuwa vitakuwa na nafasi muhimu katika kujenga urafiki na kuondoa uadui na chuki dhidi ya wafuasi wa dini na hasa dhidi ya Waislamu na Uislamu nchini Marekani. 794114
captcha