IQNA

Azhar kuanzisha tena uhusiano na Vatican

18:41 - May 23, 2011
Habari ID: 2127284
Halmashauri inayoshughulikia mazungumzo baina ya dini tofauti ya Vatican imesema kuwa Azhar iko tayari kuanzisha tena mazungumzo yake ya kidini na Kanisa Katoliki.
Ikitoa taarifa kuhusiana na suala hilo halmashauri hiyo imesema kuwa kufuatia matamshi ya hivi karibuni ya Ahmad Tayyib Sheikh wa al-Azhar kuhusiana na udharura wa kuanzishwa tena mazungumzo hayo, hivi karibuni Nabil al-Arabi, Waziri wa Mambo ya Nje wa Misri aliwakabidhi wakuu wa Vatican barua ya kutangaza msimamo wa al-Azhar kuhusu jambo hilo. Taarifa hiyo imesema kuwa Sheikh wa al-Azhar ameelezea matumaini yake ya kuondolewa matatizo yaliyopo kati ya kituo hicho muhimu cha Kiislamu na Vatican ikiwa ni katika juhudi za kuandaliwa mazingira ya kuhuishwa mazungumzo hayo.
Tunakumbusha hapa kwamba mazungumzo ya kidini kati ya vituo viwili hivyo muhimu vya kidini yalisimamishwa mwanzoni mwa mwaka huu kufuatia matamshi ya kashfa ya Papa Benedict XVI kuhusiana na hali ya Wakristo nchini Misri. 796752
captcha