IQNA

'Wiki ya Utamaduni wa Kiislamu' kufanyika Roma

22:57 - May 23, 2011
Habari ID: 2127293
Shirika la Kiislamu la Elimu, Sayansi na Utamaduni ISESCO litashiriki katika 'Wiki ya Utamaduni wa Kiislamu' iliyoandaliwa katika mji mkuu wa Italia Roma kuanzia Mei 30.
'Wiki ya Utamaduni wa Kiislamu' imeandaliwa na Manispaa ya Roma kwa ushirikiano na Kituo cha Utamaduni wa Kiislamu cha Roma.
ISESCO itawakiliwsha katika hafla hiyo na Dkt. Mohammad Yahya Pallavicini, Naibu Mkuu wa Jumuiya za Kiislamu Italia ambaye pia ni Mkuu wa Baraza Kuu la ISESCO kwa ajili ya Waislamu waishio nje ya ulimwengu wa Kiislamu.
Atawasilisha makala kuhusu juhudi za ISESCO za kustawisha mazungumzo baina ya dini na tamaduni.
797141
captcha