Hayo ni kwa mujibu wa idhini iliyotolewa na Kituo cha Fatuwa cha Wizara ya Uadilifu cha Imarati kufuatia swali lililoulizwa iwapo inajuzu kuweka Qur'ani Tukufu katika vyumba vya hoteli hasa kwa kuzingatia kuwa baadhi ya wateja si Waislamu.
"Kuweka Qur'ani katika vyumba vya hoteli ni jambo linalojuzu maadamu heshima yake inadumishwa", imesema fatuwa iliyochapishwa na gazeti la kila siku la Al Khaleej.
Fatuwa hiyo imeongeza kuwa, 'Hoteli pia zinaweza kuweka Qur'ani kwa lugha nyinginezo vyumbani kwani zinaweza kuguswa na wengine na maadamu zinaheshimiwa'.
797130