Mashindano hayo ya Qur'ani ambayo huandaliwa na Shirika la Awqaf la Iran yatawaleta pamoja maqari na mahafidh wa kimataifa wa Qur'ani Tukufu kutoka Iran na nchi zingine za Kiislamu duniani.
Mashindano hayo yanatazamiwa kuendelea hadi Julai sita na maelezo zaidi yatatolewa baadaye.
Mashindano yaliyopita yalifanyika katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano mjini Tehran na mwaka huu pia inatazamiwa mashindano hayo yatafanyika katika ukumbi huo.
796826