Kikao hicho kitafanyika Juni 25-26 kwa lengo la kuimarisha mshikamano wa kimataifa katika kupambana na ugaidi chini ya kaulimbiu ya 'Dunia Bila Ugaidi'.
Kwa mujibu wa Mohammad Hassan Saleh Maram ambaye ni Naibu Mkuu wa Idara ya Mawasiliano katika Ofisi ya Rais wa Iran, kati ya mada zitakazojadiliwa katika kongamano hilo la siku mbili ni mbinu za kupambana na ugaidi.
Maram amesema Iran imezindua mtandao wa intaneti katika www.icterrorism.com ambao una mitazamo ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kuhusu vita dhidi ya ugaidi.
807071