IQNA

Wanafunzi wa mashindano ya Qur'ani Bahrain wapongezwa

17:33 - June 13, 2011
Habari ID: 2137642
Wanafunzi wa mashindano ya hifdhi na kiraa ya Qur'ani Tukufu huko Bahrain walishukuriwa na kuenziwa katika sherehe maalumu iliyofanyika katika shule ya Kiislamu ya Ibn Haitham hapo siku ya Jumapili katika mji mkuu wa nchi hiyo Manama.
Kwa mujibu wa gazeti la Gulf Daily zaidi ya wanafunzi wa kike wapatao 300 kutoka kote nchini humo walishiriki katika hatua ya kwanza ya mashindano hayo ambapo wanafunzi 100 kati yao walichaguliwa kushiriki katika hatua ya mwisho.
Walioshinda katika hatua hiyo ya mwisho ndio walioenziwa katika sherehe iliyofanyika jana katika shule ya Ibn Haitham. 808001
captcha