IQNA

Kozi ya Sharia za Kiislamu yakamilika Pakistan

14:56 - June 22, 2011
Habari ID: 2142258
Washiriki wa Kozi ya 53 ya Akademia ya Sharia katika Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Kiislamu cha Islamabad nchini Pakistan wamepokea vyeti katika sherehe zilizofanyika Jumatatu.
Kozi hiyo ya wiki 16 iliyokuwa na anwani ya ‘Kozi ya Sheria za Kiislamu kwa Majaji na Waendesha Mashtaka’ iliwashirikisha wataalamu 12 wakiwemo majaji na waendesha mashtaka kutoka maeneo yote ya Pakistan.
Akizungumza katika hafla hiyo Rais wa Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Kiislamu cha Islamabad Dr. Mumtaz Ahmad amewapongeza washiriki kwa kufuzu katika kozi hiyo. Amesema Wapakistani wote wanatumai kuwa vyombo vya mahakama nchini humo vitafanya kazi bila kuathiriwa na mashinikizo.
812547
captcha