IQNA

Masomo ya msimu wa joto katika Msikiti Mkuu wa Abu Dhabi

14:53 - June 22, 2011
Habari ID: 2142259
Mpango maalumu wa masomo ya vijana walio na umri wa kati ya miaka 7 hadi 18 unatazamiwa kuanza kutekelezwa wiki ijayo katika Msikiti Mkuu wa Sheikh Zayed mjini Abu Dhabi nchini Imarati.
Katika masomo hayo washiriki watajifunza hifdhi ya Qur’ani Tukufu, adhan, upigaji picha na mbinu za kusoma.
Mashindano ya Qur’ani yatakuwa katika makundi mawili moja la washiriki walio na umri wa miaka 7-13 na la pili kwa walio na umri wa miaka 14-18. Aidha kutakuwa na programu maalumu kwa ajili ya wasichana.
Wataalamu kutoka Wizara ya Wakfu na Masuala ya Kiislamu ya Imarati watawasaidia watoto kufahamu sheria za kusoma Qur’ani Tukufu.
Talal al Mazroui Mkurugenzi wa Mipango katika msikiti huo amesema kuna mikakati ya kutoa mafunzo kwa kizazi cha vijana kuhusu thamani na mafundisho ya dini tukufu ya Kiislamu. 812517
captcha