IQNA

Awamu ya mwisho ya mashindano ya kimataifa ya Qur’ani kuonyeshwa al Jazeera

16:18 - June 22, 2011
Habari ID: 2142826
Awamu ya mwisho ya mashindano ya kimataifa ya kiraa ya Qur’ani Tukufu makhsusi kwa ajili ya watoto ya Qatar itaonyeshwa katika kanali ya televisheni ya al Jazeera Ijumaa ya wiki hii.
Mashindano hayo yatafanyika katika mji mkuu wa Qatar Doha.
Awamu hii ya mwisho ya mashindano hayo itafunguliwa na Waziri wa Wakfu wa Qatar Ghaith bin Mubarak na kuonyeshwa moja kwa moja katika televisheni ya watoto ya al Jazeera.
Sherehe za ufunguzi wa mashindano hayo zitashirikisha kamati ya majaji wa kimataifa wa Qur’ani na kiraa ya wasomaji watatu mashuhuri wa Qur’ani duniani.
Awamu hii ya mwisho ya kiraa ya Qur’ani ya watoto ya kanali ya televisheni ya al Jazeera itawachuanisha watoto 63 kutoka mabara matano ya dunia.
Wizara ya Wakfu na Masuala ya Kiislamu ya Qatar imetenga zawadi tano za fedha taslimu kwa washindi wa mashindano hayo yatakayosimamiwa na majaji na wataalamu mashuhuri wa sayansi ya Qur’ani kutoka nchi mbalimbali duniani. 813373

captcha