Baraza hilo linasema utafiti huo unaonyesha kuwa chuki dhidi ya Uislamu (Islamophobia) nchini Marekani imeongezeka baada ya kuchaguliwa rais Barack Obama. Makundi ya mrengo wa kulia ya chama cha Republican yamekuwa yakieneza hisia za chuki dhidi ya Waislamu na kudai kuwa sheria za Kiislamu zitatelekezwa nchini humo.
Baraza la Uhusiano wa Marekani na Uislamu lenyewe limelengwa katika chuki hizo na kudaiwa kuwa linaunga mkono ugaidi. Baraza hilo limetajwa pamoja na mashirika mengine 250 kuwa yanaunga mkono Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina Hamas.
815467