IQNA

Malaysia yautaka Umoja wa Mataifa kulinda Msafara wa Uhuru-2

18:06 - June 29, 2011
Habari ID: 2146724
Waziri Mkuu wa Malaysia Najib Tun Razak amemtumia barua Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon akimtaka kulinda Msafara wa Uhuru-2 unaoelekea Gaza kwa shabaha ya kuvunja mzingiro wa kidhamu wa Wazayuni dhidi ya raia wa eneo hilo.
Waziri Mkuu wa Malaysia amesema katika barua hiyo kwamba lengo la msafara huo ni kufikisha misaada ya kibinadamu kwa raia wa Gaza na ameutaka Umoja wa Mataifa kuwalinda watu walioko kwenye msafara huo.
Najib Tun Razak ameutaka umoja huo kuwatuma wawakilishi wake kwenda kuchunguza bidhaa zinazobebwa na meli za msafara huo na kuwahakikishia walimwegu na utawala wa Kizayuni wa Israel kwamba meli hizo zinabeba misaada ya kibinadamu.
Waziri Mkuu wa Malaysia ameongeza kuwa wanaharakati wa haki za binadamu wa Malaysia wamo katika msafara huo unaojumuisha wawakilishi wa nchi mbalimbali duniani.
Vilevile amemtaka Ban Ki-moon autahadharishe utawala ghasibu wa Israel juu ya hatari za kutumia mabavu dhidi ya meli za msafara wa Uhuru-2. 817384
captcha