IQNA

Jumba la Makumbusho la Imam Hussein AS lafunguliwa Karbala

16:04 - July 10, 2011
Habari ID: 2151789
Jumba la Makumbusho la Imam Hussein AS limefunguliwa rasmi katika hafla iliyofanyika Jumamosi usiku katika mji mtakatifu wa Karbala.
Sherehe za ufunguzi zilifanyika katika Ukumbi wa Khatamul Anbiya katika Haram ya Imam Hussein AS na kuhudhuriwa na idadi kubwa ya watu.
Mkurugenzi wa jumba hilo la makumbusho Ala Zia-U-Din amesema ufunguzi huo umefanyika kama sehemu ya sherehe za 'Machipuo ya Kufa Shahidi'. Sherehe hizo hufanyika kila mwaka katika mwezi wa Shaaban kwa mnasaba wa kukumbuka kuzaliwa Imam Hussein AS.
822549
captcha