IQNA

Semina ya Ijue Qur'ani kufanyika Dubai

15:46 - July 12, 2011
Habari ID: 2153408
Semina ya Ijue Qur'ani Tukufu itafanyika katika siku za tarehe 23 na 29 Julai katika kituo cha Waislamu wa madhehebu ya Shia Ithnaashari mjini Dubai.
Kituo cha habari cha Dubaijamaat kimeripoti kuwa semina hiyo itafanyika kwa hima ya Kamati ya Ulinganiaji ya kituo cha Shia Ithnaashari mjini Dubai katika ukumbi wa Hathrat Abbas (as).
Semina hiyo ya siku mbili itafanyika kwa mnasaba wa kukaribia mwezi mtukufu wa Ramadhani ambao ni mwezi Qur'ani ilioteremshwa ndani yake kwa lengo la kutayarisha uwanja mzuri wa kuielewa Qur'ani Tukufu kama hatua ya kwanza ya kustafidi na hazina inayotoa uhai ya kitabu hicho cha Mwenyezi Mungu.
Miongoni mwa maudhui zitakazojadiliwa katika semina hiyo ni pamoja na Qur'ani na hakika ya kitabu hicho cha mbinguni, chanzo na asili ya Qur'ani Tukufu, lengo la udharura wa kuteremshwa Qur'ani, sababu za kuteremshwa Qur'ani, ujumbe wa Qur'ani, walengwa wa Qur'ani, mashukio ya mwisho ya walioamini Qur'ani, daraja za ujumbe wa Qur'ani na kadhalika. 823948
captcha