IQNA

Muwahabi aliyetusi Ushia afungwa miaka mitatu gerezani Kuwait

13:11 - July 20, 2011
Habari ID: 2157069
Mahakama moja ya Kuwait imemhukumu kifungo cha miaka mitatu jela mfuasi wa kundi la Wahabi kwa kosa la kuyavunjia heshima madhehebu ya Shia.
Mubarak al Badhali amepatikana na hatia ya kutusi Ushia na kutisha kumuua Saleh al Ashur mbunge Mshia katika Bunge la Kuwait.
Itakumbukwa kuwa mwaka 2010 al Badhali akiwa katika kituo cha polisi alimkosea heshima Saleh Ashur na kutusi madhehebu ya Kiislamu ya Shia. Sauti ya tukio hilo ilisambazwa katika intaneti. Mubarak al Badhuli ni mhubiri wa Kiwahabi kutoka Kuwait aliye na misimamo mikali ambaye analenga kuibua hitilafu za kimadhehebu baina ya Mashia na Masuni. 828105
captcha